Maswali yaliyoulizwa mara nyingi :
Je, kuna utofauti
wowote kati ya eMikutano toleo la
kwanza na toleo la pili?
Ndio, toleo la pili inakuruhusu
kuomba mkutano kwa kutumia
web app na simu app (mobile
application)
Toleo la pili inaruhusu mtumishi
yoyote mwenye barua pepe ya
serikali kuomba nafasi ya
mkutano.
Je, Ninaweza kuomba
vikao vingapi kwa siku?
Unaruhusiwa kuomba vikao vitano
kwa siku na vinaweza kufanyika kwa
muda mmoja.
Je, kwanini tunaandika
namba za simu?
Ili kupata taarifa fupi za Mikutano yako
uombayo
Je naweza kutumia e-Mikutano
wakati wa usiku?
Ndio, mfumo wa e-Mikutano unapatikana muda
wote siku zote za juma.
Unachotakiwa kufanya ni kupanga mapema muda
wa kufanya mkutano na kisha tuma maombi ya
kuwekewa nafasi kupitia linki iliyopo kwenye
ukurasa wa kwanza wa e-mikutano
Je naweza kuwaalika
washiriki kwenye
mkutano kupitia
ukurasa wa maombi
kwa kutumia barua
pepe zao?
Ndio, utaweza kuwaalika kwa kutumia
barua pepe yoyote ya mshiriki.
Nawezaje kupata
Tokeni ya mratibu?
Tokeni ya mratibu itapatikana tu
kwenye akaunti yako ya maombi pale
tu unapoomba mkutano ili kuzuia
kupatikana kwa mtu mwingine.
Je naweza kuanzisha mkutano bila
kuomba ruhusa au kuweka nafasi
kabla
Hapana, ni muhimu kufanya maombi ya mkutano
kabla ya muda. Unashauliwa kupanga mkutano wako
mapema na kuweka nafasi kwenye mfumo siku mbili
kabla kwani waombaji ni wengi.
Je mtu yeyote anaweza tuma
maombi ya kuwekewa nafasi ya
mkutano kwenye mfumo e-
mikutano?
Hapana, mfumo huu ni kwa ajili ya
Taasisi za Umma, wanaoweza kuomba
nafasi kwenye mfumo ni
maafisa/watumishi wa serikali kupitia
barua pepe ya serikali na nywila
aliyopewa anaweza kuomba nafasi ya
mkutano.
Ni siku zipi au muda gani
ninaruhusiwa kuomba nafasi ya
kufanya mkutano?
Unaweza kuomba nafasi ya kufanya
mkutano muda wowote.
Mfumo unakuruhusu kuchagua siku,
muda wa kuanza Mkutano, kiasi cha
muda ambacho mkutano utatumia, na
idadi ya Washiriki.
Ili kufanya maombi ya nafasi ya
mkutano inanitaka niweke jina na
nywila. Je naweza kujisajili kwa
njia gani ili kupata jina na nywila
za kuingilia kwenye mfumo wa
kuombea nafasi?
Anaetakiwa kuomba nafasi ya
mkutano ni mtu yoyote mwenye
namba ya simu inayotambulika na
kutumika, barua pepe ya serikali na
nywila unazotumia kwenye Mfumo wa barua wa
serikali (Government Mail System (GMS)).
Nimeshindwa kuipata e-Mikutano
simu App kwenye Playstore na
iStore?
App ya e-Mikutano inapatikana kwenye linki iliyopo
ukurasa wa kwanza wa tovuti ya e-Mikutano.
Gonga linki hiyo na kisha pakua mfumo.
Mbona e-Mikutano App haikubali
kusakinisha (install) kwenye simu
yangu?
App ya e-Mikutano inatumika kwa simu za Android
tu na zenye mfumo endeshi (OS) kuanzia tolea la 7.
Mfumo wa e-Mikutano unatakaa
kuunganishwa kwenye kivinjari
changu.
Mfumo huu kwasasa unapatikana kwa kutumia kivinjari cha Google Chrome na Chromium.
Tufanyeje kuendelea na mkutano
kama tupo kwenye Mtandao usio
imara?
Inashauriwa kufifisha(mute) video kwa baadhi ya
wajumbe au wote na kuendelea na kuwasiliana kwa
sauti tu ili kuongeza ubora.
Naweza kuwaona washiriki wote
lakini wao hawanioni.Nini tatizo?
Angalia kama kamera yako imewashwa au kivinjari
chako kimeruhusu e-mikutano kutumia kamera
yako. Kama ruhusa imetolewa basi angalia kama
kamera yako haijazibwa na kitu na jaribu kuifuta.
Ni idadi ya watu wangapi nina
ruhusiwa kuwaalika kwenye
mkutano wangu?
Inaruhusiwa kualika mpaka watu 30
kwa mkutano mmoja. Kama kuna
ulazima wa kuwa na wajumbe zaidi ya
30 kwenye mkutano unashauriwa
kuwasiliana na dawati la msaada.
Nawezaje kuzuia mtu asiehusika
kuingia kwenye mkutano wetu?
Ni kwa kumkataa mshiriki kutoka
kwenye chumba cha kusubiria (lobby
room). Pia ni muhimu kutoa au
kugawa tokeni ya mkutano kwa
wahusika kwa kutumia njia sahihi na
yenye usiri na usalama.
Kuna muingiliano wa sauti kati ya
mtu anaeongea na zingine
zinazoleta kelele na kufanya
kutosikilizana vizuri. Nini kifanyike?
Inashauri kama mshiriki hazungumzi basi ni muhimu
kuzima au kufifisha kinasa sauti chake. Kwani kinasa
sauti kina tabia ya kuchukua sauti za mazingira mtu
alipo na kuziingiza kwenye mfumo hivyo kuleta
mchanganyiko na sauti ya mzungumza unaopelekea
kuwa na kelele.